Matukio

random/hot-posts

Habari za hivi punde

6/recent/slider

TANGAZO

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO
WAZIRI MKUU AHIMIZA MALEZI YA KIMAADILI NA USHIRIKIANO WA KIJAMII
 TARURA YAWAIMARISHA MAAFISA UNUNUZI KUDHIBITI HOJA ZA UKAGUZI
 WAZIRI MKUU AVITAKA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA KUWA MACHO DHIDI YA WAVUNJA AMANI
WAUGUZI, WAKUNGA WAHIMIZWA UTENDAJI WA MABADILIKO, KULINDA UTU WA MGONJWA
UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO
MATUMAINI MAKUBWA YATAWALA KUWA TUME YA MAJAJI WASTAAFU ITATENDA HAKI BILA UPENDELEO  Thursday, May 21, 2026    Katibu Mkuu wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Salum Mwalimu Wadau wa siasa na waliokuwa wagombea urais nchini wameonyesha kuwa na matumaini makubwa kuwa Tume ya Uchunguzi wa Kijinai iliyoundwa hivi karibuni itatenda haki kikamilifu na kuondoa kabisa hofu na malalamiko ya wananchi kuhusu uwajibikaji.  Tume hiyo, inayoongozwa na Jaji wa Mahakama ya Rufani Shabani Ally Lila akisaidiana na makamishna ambao ni majaji wastaafu Gad Mjemmas, Awadh Mohamed Bawazir, na Aishieli Sumari, inatarajiwa kufanya upelelezi wa kina ili kubaini wahusika wa ghasia, vifo, na majeraha.  Wadauhao hao wameeleza kuwa wana imani kubwa na wajumbe hao kutokana na rekodi zao za uadilifu, wakiamini kuwa watafanya kazi kwa mujibu wa sheria ili kuleta majibu yataridhisha na kuweka wazi ukweli utakaotibu majeraha ya kijamii.  Aliyekuwa mgombea urais kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMA), Salum Mwalimu, ameeleza matumaini yake kuwa kuwepo kwa tume hiyo kutasaidia kuanza kwa uwajibikaji wa kweli, hatua itakayofanya mioyo ya watu ipoe na kurejesha utayari wa wananchi kushirikiana kama taifa moja.  Kwa upande wake, aliyekuwa mgombea urais kupitia Chama cha UMD, Mwajuma Mirambo, aliongeza kuwa wana matumaini makubwa kwa sababu chombo hicho kimeundwa na watu sahihi watakaosikiliza maoni ya wanajamii na kuleta mwarobaini wa jinsi ya kujenga taifa lenye umoja na amani.  Ili tume hiyo iweze kutenda haki na kufanya kazi yake kwa ufanisi, viongozi hao wametoa wito kwa Watanzania kuwa watulivu na kuepuka kuendesha midahalo inayoweza kuingilia au kuvuruga mwenendo mzima wa uchunguzi huo wa kijinai.
 WAZIRI MKUU ATATUA MGOGORO WA ARDHI ULIODUMU KWA MIAKA 51 WILAYANI ROMBO
WAUGUZI, WAKUNGA IMARISHENI HUDUMA ZENYE UTU NA STAHA
 MWENYEKITI WA BARAZA LA VYAMA VYA SIASA NA WADAU WAHIMIZA MARIDHIANO BILA MASHARTI
TRILIONI 4.2 KULINDA MIPAKA: SERIKALI YAANIKA MKAKATI KABAMBE WA KUIMARISHA ULINZI WA TAIFA
WAMERUDI NYUMBANI BINADAMU ALIPOANZIA

Follow Us On Instagram