
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Balozi, Dkt. Pindi Chana (Mb) akiwasili katika Ofisi za Makao Makuu ya Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) jijini Dar es Salaam leo Februari 19,2025 kwa ziara ya kikazi.
Mhe. Chana alipokelewa na Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania, Bw. Ephraim Mafuru, Mwenyekiti wa Bodi ya Utalii Tanzania, Mhe.Balozi, Dkt.Ramadhani Dau, Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt.Hassan Abbasi, Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii (anayeshughulikia Utalii ) Nkoba Mabula na Mkurugenzi wa Idara ya Utalii, Dkt.Thereza Mugobi.


