Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Mhe. Dkt. Tulia Ackson, leo tarehe 4 Mei, 2025 amefungua na kufunga rasmi Kongamano la Wanawake wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) lililofanyika Jijini Dar es salaam kwa kuwakutanisha zaidi ya wanawake 1000 wa Shirika hilo.
Katika hotuba yake pamoja na mambo mengine, Dkt. Tulia amewasisitiza wanawake ya kuwa hawapaswi kujidharau hususani katika kipindi hiki ambacho taifa la Tanzania linaongozwa na Rais mwanamke ambaye ni Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na badala yake wanapaswa kuinuka na kuonesha uwezo wao kwa jamii.