TANGAZO

TANGAZO

FLIGHTLINK KUZINDUA SAFARI ZA NDEGE ZA KILA SIKU KWENDA NAIROBI WIKI IJAYO



Shirika la ndege la Flightlink, limetangaza kuanza kwa safari za kila siku kutoka Tanzania hadi Uwanja wa Ndege wa Wilson jijini Nairobi, kuanzia Juni 15, 2025. Mpango huu unalenga unaunga mkono juhudi za serikali ya Tanzania kukuza utalii, kama ilivyosisitizwa na Rais Samia Suluhu Hassan wakati akizindua filamu ya Royal Tour.



Safiri hizi mpya ambazo zitaanza wiki ijayo, zinasaidia kwa kiasi kikubwa kukuza utalii na biashara kwani watalii na wafanyabishara wataweza kusafiri kwa urahisi kwenda Nairobi (Wilson Airport).


Kwa kushirikiana na Wizara ya Utalii na Bodi ya Watalii Tanzania, Flightlink inalenga kuimarisha usafiri wa watalii kati ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ya Tanzania na Hifadhi ya Maasai Mara ya Kenya. Vikiwa kama lango kuu, vituo vya Flightlink vilivyoko Arusha na Uwanja wa Ndege wa Wilson wa Nairobi vitarahisisha usafiri kwa wale wanaotamani kuona wanyamapori katika nchi zote mbili.


Sanjari na uzinduzi huu, hii itakuwa ni hatua kubwa - kufunguliwa kwa Uwanja wa Ndege wa Arusha kama kitovu cha forodha na uhamiaji kwa ajili ya uendeshaji wa ndege za aina ya Turbo-prop. Maendeleo haya yanawakilisha hatua kubwa mbele katika kuimarisha muunganisho wa kikanda na kutoa uzoefu rahisi wa kusafiri.


"Tunafuraha kuzindua njia hii mpya na kuchangia ukuaji wa sekta ya utalii nchini Tanzania na Kenya," alisema Munawer Dhirani, Mkurugenzi Mkuu - Flightlink. "Ushirikiano wetu na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania na Bodi ya Utalii Tanzania unasisitiza dhamira yetu ya pamoja ya kutangaza maajabu ya asili na urithi wa kitamaduni wa eneo hili."


Safari za ndege za kila siku zitawapa abiria ratiba inayofaa, na kuongeza ratiba zao za safari. Ndege za kisasa za Flightlink za ATR na Cessna na viwango vya huduma ya kiwango cha juu huhakikisha safari yenye burudani na ya kufurahisha.


Hata hivyo, Flightlink inatoa shukurani zake kwa Wakurugenzi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania, pamoja na Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi na mamlaka husika za viwanja vya ndege nchini Kenya, kwa msaada na ushirikiano wao katika kufanikisha safari hii. Juhudi zao zimekuwa muhimu katika kuwezesha uzinduzi wa huduma hii mpya.


"Kwa maelezo zaidi kuhusu ratiba za safari za ndege, nauli, na kuhifadhi, tafadhali tembelea www.flightlink.co.tz," MD wa Flightlink anahitimisha.


Kama una Taarifa,Picha, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kwa simu +255 766 166 125 au Email : emmymwaipopo@gmail.com