Mhe. Naibu Waziri wa Mali Asili na utalii Mhe. Dustan Kitandula (Mb) Juni 20, 2025 ametembelea banda la NCAA lililopo ndani ya Banda la Wizara ya Mali asili na Utalii kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea jijini Dodoma katika Viwanja vya Chinangali Park.
Akiwa ndani ya Banda hilo, Mhe. Kitandula ametoa wito kwa NCAA kuendelea kutoa Elimu kwa umma kuhusiana na jamii inayoishi ndani ya Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro kwa kulezea historia na asili halisi ya jamii hiyo.
Aidha, Naibu Waziri amewahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi kutembelea banda hilo la Wizara ya Maliasili na Utalii ili kupata elimu kuhusu shughuli za uhifadhi pamoja na fursa mbalimbali za uwekezaji zinazopatikana katika sekta ya utalii.
Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kwa mwaka huu yalianza rasmi Juni 16, 2025, na yanatarajiwa kufikia kilele chake Juni 23, 2025, yakihusisha taasisi mbalimbali za umma zikiwemo zile zilizopo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii.