TANGAZO

TANGAZO

TUME YAVIHIMIZA VYOMBO VYA HABARI KURIPOTI HABARI ZA UCHAGUZI KWA USAHIHI

 

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kikao cha Tume na Wahariri wa Vyombo vya Habari kuhusu uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Kikao hicho cha siku moja kilifanyika jijini Dar es Salaam leo Agosti 01, 2025. 
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kikao cha Tume na Wahariri wa Vyombo vya Habari kuhusu uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Kikao hicho cha siku moja kilifanyika jijini Dar es Salaam leo Agosti 01, 2025. 
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Ndg Kailima Ramadhani akitoa mada wakati wa Kikao cha Tume na wahariri wa Vyombo vya Habari kuhusu uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Kikao hicho cha siku moja kilifanyika jijini Dar es Salaam leo Agost 01, 2025. 
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Ndg Kailima Ramadhani akitoa mada wakati wa Kikao cha Tume na wahariri wa Vyombo vya Habari kuhusu uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Kikao hicho cha siku moja kilifanyika jijini Dar es Salaam leo Agost 01, 2025. 

Sehemu ya Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari wakishiriki mkutano wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na Wahariri wa Vyombo vya Habari kuhusu Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 uliofanyika jijini Dar es Salaam leo Agosti 01, 2025. 
Na Waandishi Wetu
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imevihimiza vyombo vya habari nchini kuripoti kwa usahihi na kwa wakati kuhusu taarifa zote zinazohusu Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, ili kuwawezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika mchakato wa uchaguzi.

Kauli hiyo imetolewa leo, tarehe 1 Agosti 2025, jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Tume hiyo, Mheshimiwa Jaji wa Mahakama ya Rufani Jacobs Mwambegele, wakati wa ufunguzi wa mkutano kati ya Tume na Wahariri wa Vyombo vya Habari.

Jaji Mwambegele amesema vyombo vya habari vina nafasi muhimu katika kuhakikisha wananchi wanapata elimu ya mpiga kura na taarifa sahihi zinazowawezesha kufanya maamuzi ya msingi kwa uhuru na kwa amani.

Aidha, amewasihi Wahariri wa vyombo vya habari kutumia majukwaa yao kuwaelimisha na kuwahamasisha wananchi waliojiandikisha kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kujitokeza kwa wingi kupiga kura siku ya uchaguzi mkuu, utakayofanyika tarehe 29 Oktoba 2025.

Amesisitiza kuwa ushirikiano kati ya Tume na vyombo vya habari ni nguzo muhimu katika kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani na kwa kuzingatia sheria za uchaguzi.

Akitoa mada kuhusu Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025, Mkurugenzi wa Uchaguzi Bw. Kailima Ramadhani amesema vyombo vya habari vina nafasi ya kipekee katika kufanikisha maandalizi na uendeshaji wa uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Ameongeza kuwa, katika nchi yoyote inayodhamiria kufanikisha jambo kubwa kama uchaguzi, vyombo vya habari ndio msingi wa kwanza, kwani kupitia kwao, wananchi hupata taarifa sahihi, zilizofanyiwa utafiti na kuhakikiwa.

Bw. Kailima amesema kuwa bila ushirikiano wa karibu na vyombo vya habari, juhudi zote za Tume katika kutoa elimu na taarifa kwa umma haziwezi kuwafikia walengwa. 

"Maana yake kila kinachotolewa na Tume hakiwezi kuwafikia wananchi iwapo vyombo vya habari havitaamua jambo hilo lifanikiwe," amesema.
Ameongeza kuwa wadau wote wa uchaguzi, vikiwemo vyama vya siasa, wanategemea vyombo vya habari kutoa taarifa zitakazowawezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika mchakato wa uchaguzi.

Amesisitiza kuwa vyombo vya habari ndivyo vinavyoweza kuwa sauti ya kwanza ya kuonesha upotoshwaji wa aina yoyote unaofanywa kwa bahati mbaya au kwa makusudi kuhusu Tume na kuhusu zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025.

“Tunawaomba na kuwanasihi, kutumia nafasi na fursa mlizonazo kuhakikisha kunakuwepo na taarifa za mara kwa mara za kuelezea kinachoendelea kuhusu uchaguzi,” amesisitiza Mkurugenzi wa Uchaguzi.

Aidha wahariri hao wamekumbushwa kutumia kauli mbiu ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 ambayo ni “Kura Yako Haki Yako Jitokeze Kupiga Kura” kwenye taarifa zao wanazozitoa kwa umma ikiwa ni sehemu ya uhamasishaji kwa wananchi kujitokeza kupiga kura.
Sehemu ya Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari wakishiriki mkutano wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na Wahariri wa Vyombo vya Habari kuhusu Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 uliofanyika jijini Dar es Salaam leo Agosti 01, 2025. 

Sehemu ya Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari wakishiriki mkutano wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na Wahariri wa Vyombo vya Habari kuhusu Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 uliofanyika jijini Dar es Salaam leo Agosti 01, 2025. 

Sehemu ya Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari wakishiriki mkutano wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na Wahariri wa Vyombo vya Habari kuhusu Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 uliofanyika jijini Dar es Salaam leo Agosti 01, 2025. 

Sehemu ya Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari wakishiriki mkutano wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na Wahariri wa Vyombo vya Habari kuhusu Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 uliofanyika jijini Dar es Salaam leo Agosti 01, 2025. 

Kama una Taarifa,Picha, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kwa simu +255 766 166 125 au Email : emmymwaipopo@gmail.com