Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Edward Mpogolo, akisalimiana na Kamishna wa Fedha na mipango Jeshi la Magereza CP. Chacha Binna Jackson katika viwanja vya Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania (TCTA), Ukonga jijini Dar es Salaam, leo Septemba 4, 2026, wakati akiwasili kwa ajili ya kushiriki Hafla ya Kufunga Mafunzo ya Kozi ya Uongozi Daraja la Kwanza (SGT No.1) ya mwaka 2026.






