TANGAZO

TANGAZO

KAMATI YA BUNGE YATUA NGORONGORO KUKAGUA MIRADI

 


Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, ikiongozwa na Mwenyekiti wao, Mhe. Timotheo Mnzava  wakiambatana na Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Balozi, Dkt. Pindi Chana na Naibu  wake Mhe. Dunstan Kitandula pia Naibu Katibu Mkuu wa Maliasili na Utalii, Kamishina wa Polisi Benedict Wakulyamba wamekagua ujenzi wa Ofisi mpya za Hifadhi ya Ngorongoro iliyojengwa nje ya Hifadhi.


Utekelezaji wa mradi huo wa gharama   ya takribani  shilingi   bilioni 10. 5 wa Ofisi na miundombinu mbalimbali umefikia  asilimia  85 na unatarajiwa kukamilika Mei 30, 2025.


Kamati ipo katika siku ya pili ya ukaguzi wa miradi mbalimbali ya taasisi chini ya Wizara hiyo kwa siku tatu katika Mkoa wa Manyara na Arusha.



Kama una Taarifa,Picha, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kwa simu +255 766 166 125 au Email : emmymwaipopo@gmail.com