TANGAZO

TANGAZO

WAZIRI MCHENGERWA ASHIRIKI KONGAMANO LA UCHUMI LA ARUSHA

 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa ni miongoni mwa viongozi waliohudhuria jukwaa la uchumi Arusha linalofanyika katika Ukumbi wa IACC Arusha.


Kongamano hili limejumuisha zaidi ya wadau 1000 kutoka maeneo mbalimbali duniani na kushirikisha mawaziri kadhaa wa sekta za tofauti.


Mwanamajumui wa Afrika Profesa Patrick Lumumba pia amealikwa kuwa miongoni mwa watoa mada.


Jukwaa hilo limeandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda ili kutoa fursa kwa wafanyabiashara wa Mkoa huo kupata ujuzi wa namna ya kutumia fursa za uchumi zilizopo mkoani Arusha.

Kama una Taarifa,Picha, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kwa simu +255 766 166 125 au Email : emmymwaipopo@gmail.com