Watanzania na hasa vijana wanatakiwa kuunganisha nukta ambazo mara nyingi watu wanashindwa kuziona na kushabikia uasi wakisahau kwamba kuna uhusiano mkubwa wa amani na kujipatia elimu ya juu, uzalishaji wa ndani, na nguvu ya Shilingi ambayo hutengeneza uchumi wa mtu mmmoja mmoja na kisha taifa.
Kiukweli uzalishaji ndio uhai wa sarafu: Huwezi kuwa na fedha imara kama nchi yako haizalishi wataalamu. Profesa Mkenda anapozungumzia trilioni moja ya HEET, hapo anazungumzia kutengeneza "viwanda vya akili" ambavyo vitazalisha bidhaa na huduma, na hivyo kuipa thamani Shilingi yetu bila kutegemea misaada na huili linawezekana kwenye utulivu na hakuna ghasia wala uasi.
Ndio kusema katika siasa za kijiopolitika (kama tulivyoona kwenye mfano wa Venezuela na Greenland), nchi yoyote isiyo na utulivu wa ndani wa kiuchumi ni rahisi kuyumbishwa. Kwa kuwekeza kwenye elimu inayozalisha ajira (kujiajiri), serikali inakata mzizi wa malalamiko na uchochezi kwa kutengeneza vijana wenye tija.
